
Naibu
Waziri wa Afya Dkt. Kebwe Steven Kebwe akiongea na waandishi wa habari
eneo la uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere wakati wa
kupokea na kukabidhi vifaa vya kupima dalili za ugonjwa wa Ebola.
Wengine ni Mkurugenzi Msaidizi wa Kitengo cha Dharura na Maafa (kulia)
na Kaimu Mkurugenzi wa Bohari ya Dawa (MSD), Cosmas Mwaifani.
Vifaa hivyo vinavyohusisha kamera 4 zenye uwezo wa kubaini joto la
mwili wa msafiri kwa umbali wa mita 100 bila kumgusa muhusika
vimewasili leo katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius
Nyerere jijini Dar es salaam kutoka nchini Afrika ya Kusini
vilikonunuliwa.
Akikabidhi vifaa hivyo kwa wataalam wa Wizara ya Afya na Ustawi wa
Jamii, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Kebwe Steven Kebwe
amesema kuwa kuwasili kwa vifaa hivyo ni moja ya juhudi za Serikali za
kuhakikisha kuwa wananchi wanakuwa salama kwa kuuzuia ugonjwa huo
kuingia nchini.

Moja
ya kamera kati ya nne zilizoagizwa na Serikali kupimia dalili za
ugonjwa wa Ebola maeneo ya viwanja vya ndege. Kifaa hicho kina uwezo wa
kutunza picha na kumbukumbu za msafiri, muda , joto la msafiri, tarehe
aliyoingia nchini pia uwezo wa kupata takwimu kutoka kwenye hali ya
majimaji au jasho la binadamu pindi kinapoelekezwa kwake.
Amesema vifaa hivyo vitapelekwa katika maeneo ya viwanja vya ndege
na maeneo yanayotumiwa na raia wa kigeni kuingia nchini vikiwemo vya Dar es salaam, Zanzibar, Kilimanjaro,Mbeya na Mwanza.
na maeneo yanayotumiwa na raia wa kigeni kuingia nchini vikiwemo vya Dar es salaam, Zanzibar, Kilimanjaro,Mbeya na Mwanza.
Ameongeza kuwa Serikali inaendelea na mpango wa kuagiza vifaa zaidi
vya kuwezesha shughuli ya upimaji wa afya kwa wasafiri wanaotembea
(scanners) zitakazowezesha kubaini afya za wasafiri wengi zaidi kwa
wakati mmoja bila kulazimu kuwasimamisha.
Aidha, amewataka wataalam hao wa afya kufanya kazi zao kwa weledi
mkubwa kwa kuhakikisha wanawapima abiria wote wanaotoka nje ya nchi bila
kujali hadhi walizonazo ili kuweza kubaini kama wana maabukizi au
dalili za ugonjwa wa Ebola.
“Nataka mfanye kazi yenu kwa kuzingatia weledi wa taaluma yenu na kwa
kuzingatia yale mliyojifunza,mvitumie vifaa hivyo kupima kila abiria
ili kubaini joto lake bila kujali cheo wala hadhi yake maana janga hili
ni kubwa,” amesema Dkt. Kebwe.
No comments:
Post a Comment