Saturday 10 August 2013

Msimu mpya wa shindano la kuimba la Epiq Bongo Star Search ya tarajia kusajili washiriki zaidi ya 50,000



Kampuni ya simu za mikononi ya Zantel, imezindua msimu mpya wa shindano la kuimba la Epiq Bongo Star Search, mwaka huu ikiwa imejipanga kuwapa vijana wengi zaidi fursa ya kuonyesha na kuendeleza vipaji vyao.






Riya Paulsen



Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Benchmark Production, Rita Paulsen msimu huu wa saba toka shindano hilo lianzishwe mwaka 2006, kuna vitu vingi vipya ikiwamo ongezeko la jaji mmoja ambaye ni mdau wa muziki kutoka mkoa husika.
Naye Afisa Biashara mkuu wa Zantel, Sajid Khan alisema uzinduzi huo ni furaha kwa kampuni hiyo kwani unaashiria ufunguzi wa milango ya kuwasaidia vijana wengi wa Kitanzania kutimiza ndoto zao.
“Mwaka jana pekee Epiq BSS ilifanikiwa kusaili vijana zaidi ya elfu hamsini, jambo ambalo linaloonyesha kuna uhitaji wa kuwekeza zaidi katika kuwaendeleza vijana’ alisema Khan.
Katika kuwapa fursa vijana ambao hawatafikiwa na majaji, Zantel kwa kushirikiana na Push Mobile watafungua laini za kurekodi kwa simu.

No comments:

Post a Comment