Friday 8 August 2014

DIAMOND Platinumz AMETIMUA NA MAPRODUCER

Naseeb Abdul ‘Diamond Platinumz’, Nyota wa muziki wa Bongo fleva,amesema licha ya kutafuta video zenye kiwango, pia dharau 
na mapozi ya watayarishaji wengi wa Tanzania yamechangia 
kuacha kutengeneza kazi zake nchini.Akizungumza jijini Dar es Salaam juzi kabla ya kwenda nchini Canada, Diamond alisema mtayarishaji unalipahela kwanza ndio anakufanyia kazi zako, lakini watayarishaji wa hapa nchini ukishawalipa, kinachofuata ni usumbufu katika kukamilisha kazi.

Siwezi kumlipa mtayarishaji milioni 40 alafu aniletee dharau, hajui hiyohela nimeipata vipi. Wengi wao wamekuwa na dharau kama vile wanafanya kazi bure, ndiyo maana nimekuwa nikifanya kazi nje ya nchialisema Diamond.

Akifafanua zaidi, alisema unaweza ukamweleza mtayarishaji mfike studio saa 12 asubuhi, lakini atakuja saa nne.Kwangu hizo ni dharau, kama unaweza kuachana naye, yaani ukishamlipa hela ndiyo kabisa ni mapozi tu alisisitiza.Diamond, mmoja wa nyota mahiri wa muziki wa Bongo fleva nchini, kwa sasa anatamba na ngoma yake ya ‘Mdogomdogo’ aliyoifanyia nchini Afrika Kusini chini ya mtayarishaji mahiri, Godfather.

No comments:

Post a Comment