Friday 8 August 2014

NAPE MNAUYE: AZUNGUMZIA JUU YA MIDAHALO INAYOENDELEA



                             TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Katika Mdahalo ulioandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere, uliofanyika tarehe04/08/2014 mjini Dar es salaam, aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko yaKatiba Mzee Joseph Sinde Warioba na baadhi ya wajumbe wenzake pamoja na mambomengine, walikitupia lawama nyingi Chama Cha Mapinduzi na Mwenyekiti wake RaisJakaya Kikwete kwa hisia nyepesi, dhaifu na za kutunga.Mara kadhaa na hata katika mdahalo uliopita, baadhi ya waliokuwa wajumbe wa Tumeya Warioba wamekuwa wakitumia muda mwingi kujaribu kupotosha umma nakuwashambulia wote wenye mitazamo tofauti na ya kwao.Inaelekea baadhi ya wajumbe wa Tume ya Warioba wameufanya mchakato wa Katibakuwa mali yao na kufanya kila juhudi za kujitengenezea hati miliki ya Katiba.Katika mazungumzo yake Mzee Warioba na wenzake wamekuwa wakitumia takwimukutetea hoja ya serikali tatu. Lakini hivi sasa wanahama na kusisitiza kuwa ni busarazao ndizo zilizopelekea kupendekeza muundo wa serikali tatu. Kimetokea nini?La kusikitisha zaidi ni kuwa; wamekuwa na msimamo mkali usiokubali kusikiliza nakutoa nafasi kwa mawazo yoyote yanayotofautiana na ya kwao. Badala yake wanatumia juhudi kubwa kuwalazimisha Watanzania kukubaliana na maelezo yao hata kamayanaipeleka nchi pabaya.

No comments:

Post a Comment